UFUGAJI WA KUKU WA NYAMA HATUA KWA HATUA



Ufugaji wa kuku wa nyama hatua kwa hatua
  Hatua kwa hatua za ufugaji bora wa kuku wa nyama tangu kifaranga hadi kuchinjwa au kuingizwa sokon

  Madhumuni ni kukuwezesha wewe mfugaji kupata kuku bora wenye uzito sahihi ,kukuwezesha wewe kupata faida mzuri,Hivyo basi unatakiwa kujua ya kwamba wiki mbili za kwanza za uleaji wa kuku wa nyama unatakiwa kuwa mwangalifu sana

Mambo ya kuzingatia kabla hujaingiza vifaranga wako bandani

Safisha banda la kuku pamoja na mazingira yanayolizunguka yawe safi ikiwa ni pamoja na vyombo vya maji na chakula visafishwe kwa maji safi na salama kwa dawa ili kuuwa vimelea vinavyoweza kusababisha magonjwa

Hakikisha sehemu ya kuwekea vifaranga inapaswa kuwa na joto saa moja kabla hujaingiza vifaranga wako bandani
Kwa matokeo chanya hakikisha vifaranga wanafikishwa bandan haraka iwezekanavyo na kama kuna uwezekano wape chakula na maji muda huo huo
 Na usisafirishe vifaranga ukiwa umeweka kwenye buti ya gari,mara nyingi wanasafirishwa wakiwa wamewekwa kwenye siti ya gari ili wapate hewa ya kutosha na kuepuka vifarannga kupata stress au kuchoka

   Mambo ya kuzingatia baada ya vifanga kufika bandan
   Baada ya kufika tuu bandani unatakiwa uwaondoe vifaranga kwenye box mara moja ,Unapowachelewesha kwenye box hupelekea vifaranga kupata stress na hatimaye hufa au kutokukuwa vizuri
   Kwa siku saba za mwanzo wape mwanga kwa saa 23,ili kuwafanya vifaranga kuzoea mazingira mapya na kuweza kula chakula vizur bandani
 Wape chakula na maji mara tuu uwawekapo bandani ,hakikisha unaongeza vitamin au gucose kwenye maji kabla hujawapa vifaranga wako

   Hakikisha unaweka vyombo vya chakula na maji vya kutosha kulingana na kuku ulionao ili kuwawezesha vifaranga kula na kunywa maji bila shida yoyote
 
      Joto
Banda lako linatakiwa kuwa na joto la kutosha na unaweza kupima joto kwa thermometer
   Joto sahihi kwa vifaranga linatakiwa liwe kati ya 40-41 degree centigrade,unaweza pia kupima joto la kuku kwa kuchukuwa mguu wa kuku na kuuweka shavuni na shingoni mwako ukisikia mguu una joto ujue kuku wana joto la kutosha na ukisikia mguu una baridi ujue kuku wanahitaji kuongezewa joto
    Joto ni muhimu sana kwa uleaji wa vifaranga kwa wiki ya kwanza hivyo ni vyema kulifatilia kila siku ili kuepuka vifo visivyotarajiwa
   Unashauriwa kuwapima uzito vifaranga/kuku wako kila wafikishapo siku ya 7,14,21,28 na 35

            Maji

Mabadiliko yoyote katika unywaji wa maji  ni kiashiria tosha kwamba maji yanavuja,kuna tatizo kwenye chakula au ugonjwa
   Kuku kutokunywa maji vizur ni kiashiria tosha kuwa kuku wako wana shida
    Kwa kawaida inatakiwa drunker 4 kwa kuku 100 na maji yawe safi na salama na yanakuwepo kwa bandan kwa muda wote wa saa 24 na ieleweke kwamba upungufu wa maji hupelekea kuku kudumaa

     Chakula
Chakula kinatakiwa kiwekwe kwenye vyombo safi na salama na ambovyo vifaranga vinaweza kula bila shida yoyote kwa siku saba za mwanzo,baada ya hapo anza kuweka chakula kwenye feeders
  Kwa feeders za kawaida inashauriwa kuweka feeders 3 kwa kuku 100 na hakikisha chakula kinahifadhiwa sehemu salama na mbali na mwanga,panya na majimaji,epuka kuwapa kuku chakula chenye unyevunyevu na fangasi wa chakula

    Aina ya chakula kwa vifaranga

             Chick stuster
Wape 0.kg kwa kifaranga kimoja kwa muda wa wiki mbili 2

       Grower
Wape 1.5kg chakula cha ukuaji kwa vifaranga kwa wiki 2 ,na hii itakuwa ni wiki ya pili tangu umeleta vifaranga wako

       Finisher
Wape 1.5kg chakula cha umaliziaji kwa muda wa wiki mbili kabla ya kuwachinja au kuwauza

     Broiler tips
Siku 1-5
Wape glucose na mchanganyiko mmojawapo kati ya hii ifuatayo
  Neoxyvital au ctc plus typhorium au trimazin
Fluban na vitamin kama vile broiler boost aminovit au supervit au vitalyte

   Kwenye chakula
Weka vigrostat ambayo ina ridocox kwenye chakula,kilo moja kwa mfuko kuanzia wiki ya 1-4 ili kuzuia cocidiossis na wiki moja kabla ya kuwauza kwa nyama
   Siku ya 6 vitamin Critastress
    Siku ya 7
Wape chanjo ya Newcastle masaa mawili baada ya hapo endelea na maji ya vitamin (vitastress)

   Wiki ya pili
Chanjo ya Gumboro masaa mawili halafu endelea na maji ya vitamin
 
    Wiki ya tatu
Wape doxycol  au 20 % au fluban na ambrolium ,au vitalyte ,molases kwa siku 5-7

      Wiki ya nne
Hakikisha kuku wanakuwa kwenye dozi kubwa ya vitamin (vitastress)/vitalyte /broiler boost/supervit broiler

  Siku ya tano
Hakikisha kuku wanakuwa kwenye dozi ndogo ya vitamin

Wiki ya sita
Wape kuku maji ya vitamin asubuhi na maji matupu jion
 Baada ya hapo kuku wako watakuwa tayari kwa kuchinjwa au kuingizwa sokoni kwa mauzo

Ukizingatia hayo hakika utapata matokeo mazuri kwenye ufugaji wako au kama ukiona kuna tatizo zaidi mwone daktari wa mifugo kwa ushaur zaidi
     Nakutakia ufugaji mwema wenye mafanikio
        Kwa elimu zaidi bofya link
https://chat.whatsapp.com/7BXGRSO9DwYFoEaiESaoFq
  Kuingia darasan
Au wasiliana na mm kwa namba
  +255753637565
   Sofia Mutashobya
      By kwa sasa

Comments

Popular posts from this blog

UTENGENEZAJI WA ICE CREAM ZA UBUYU

JINSI YA KUTENGENEZA SABUNI YA MAGADI

JINSI YA KUANDAA UNGA WA LISHE