JINSI YA KUTENGENEZA FOUNDANT YA KEKI

NAMNA YA KUANDAA FOUNDANT KWA AJILI YA KEKI

Mahitaji

. Icing sugar, ilochekechwa vikombe 7 1/2
. Maji ya baridi 1/4 kikombe
. Unflavored gelatic kijiko 1 chakula (kwa waislam hakikisha ni halal gelatin)
. Glucose 1/2 kikombe
. Glycerine kijiko 1 1/2 chakula
. Vanilla kijiko 1

NAMNA YA KUTAYARISHA

1. Tia icing uliochekecha katika bakuli kubwa kisha weka kishimo kati

2. Katika kisufuria kidogo tia maji kisha nyunyiza gelatin juu acha ilainike kwa muda wa dk 5.

3. Ipashe moto gelatin ukiwa wakoroga hadi hadi iyeyuke yote , usiache ikachemka. Zima jiko kisha tia glucose na glycerine na koroga vizuri hadi vichanganyike.

4. Tia radha, kisha mimina katika kishimo ulichoweka katika icing yako na changanya hadi icing yote ichanganyike vizuri.

5. Kanda foundant yako katika sehemu ya kukandia au sinia hadi iwe smooth na soft, ukiona inanata ongeza icing kidogo.

6. Fanya duara kisha zungusha vizuri na plastic na tia katika container lenye mfuniko.


Usiweke katika fridge tumia kwa muda wa wiki 2
Ni vyema uiache ikae kwa muda wa masaa 8 kabla ya matumizi

Mahitaji yanapatikana maduka ya vifaa vya keki,na supermarket.

Natumaini umefurahia mafunzo haya usisite kuwasiliana nami kwa namba

0753637565/0714793386

Karibu sana

Comments

Popular posts from this blog

UTENGENEZAJI WA ICE CREAM ZA UBUYU

JINSI YA KUTENGENEZA SABUNI YA MAGADI

JINSI YA KUANDAA UNGA WA LISHE